Tunayo furaha kubwa kukukaribisha kwenye Idara ya Watoto, mahali ambapo mioyo midogo inakutana na upendo wa Yesu Kristo kwa njia ya furaha na mafundisho. Katika idara hii, tunatumia mbinu za kipekee kama michezo (Games) na hadithi za Biblia ili kuwafundisha watoto Neno la Mungu kwa njia rahisi na yenye kuvutia.
Lengo letu ni kuwajengea watoto msingi wa kiroho unaowawezesha kumjua Yesu Kristo, kuwa na maadili bora, na kukua wakiwa wafuasi wa kweli wa Bwana. Hapa, watoto wanapata fursa ya kushiriki, kujifunza, na kufurahia safari ya kiroho kwa pamoja.